Karibu

Ebenezer International Church

Hata Sasa Bwana Anatusaidia

LIVE

Tazama Mahubiri

Dira Yetu

Kutimiza agizo kuu kwa kuhubiri Habari Njema, kutoa msaada wa kiroho na kimwili, ili kuunda jamii yenye hofu ya Mungu na inayoishi kwa kufuata sheria na mamlaka.

DHIMA YETU

Kuleta mabadiliko ya maisha kwa kuhubiri Neno la Mungu na kuwasaidia watu kujiandaa kwa ajili ya maisha ya milele.

Karibu Ebenezer International Church

Ebenezer International Church (E.I.C) ni kanisa la Kipentekoste linaloongozwa na Roho Mtakatifu na limesajiliwa rasmi chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Tanzania kwa namba ya usajili S.A.23229. Makao makuu ya kanisa yapo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma, na lina matawi mbalimbali ndani ya nchi chini ya uongozi wa Askofu Mkuu Genoveva Charles Ntumo.

Kanisa lilianza mwaka 2011 kama huduma ya maombi na maombezi, na baadaye kuwa kanisa kamili tarehe 12 Julai 2020. Imani kuu ya kanisa ni juu ya Mungu mmoja katika Utatu Mtakatifu – Baba, Mwana na Roho Mtakatifu (Waefeso 4:6).

Tunajitoa kwa moyo katika kuhubiri Habari Njema ya wokovu, kubadilisha maisha ya watu kiroho, na kuwahudumia jamii kijamii na kimwili kupitia idara mbalimbali na mipango ya huduma.

Idara za Ebenezer International Church

Ili kutekeleza kwa ufanisi dhamira ya kuhubiri Injili na kuhudumia jamii kwa upana, Ebenezer International Church imeunda idara mbalimbali zinazoratibu shughuli za kiroho, kijamii na kiutawala. Kila idara ina jukumu mahsusi la kusaidia katika kuimarisha huduma ya kanisa na jamii kwa ujumla.

Idara ya Uchungaji

Idara hii inahakikisha huduma zote za kiroho, kiutawala, na kijamii zinapangwa, kuratibiwa, na kutekelezwa kwa ufanisi kwa lengo la kufanikisha maono

Idara ya Uongozi na Katibu

Idara hii inahakikisha kila shughuli inafanyika kwa mpangilio, uwazi, na kwa kufuata kanuni na maadili ya kanisa

Idara ya Fedha

Idara hii inasimamia rasilimali za kifedha, uhasibu, na shughuli zote za utawala ili kuhakikisha kanisa linafanya kazi kwa uwazi, usahihi na ufanisi.

Idara ya Mipango na Ujenzi

Idara hii inahakikisha mipango yote ya maendeleo ya kanisa inatekelezwa kwa mpangilio mzuri,

Idara ya Wanawake

Idara hii ipo chini ya uongozi wa Tedy Filimon Jacobo, ambaye anasimamia na kuratibu shughuli zote za wanawake katika kanisa

Kitengo cha Maombi na Maombezi

Kitengo hiki kinahakikisha maombi na maombezi vinaendelezwa kwa utaratibu, viwe na mshikamano, na vinachangia ukuaji wa kiroho wa waumini na maendeleo ya kanisa

Idara ya Uinjilisti, Maombi, Umisheni na Kuabudu

Idara hii ina Jukumu la kuhakikisha kwamba injili ya Yesu Kristo inafikishwa kwa watu wote, kanisa linaendelea kusimama imara katika maombi....

Idara ya Watoto na Vijana

Idara hii ina jukumu la kuhakikisha kwamba watoto na vijana wanalelewa katika msingi imara wa kiroho na kijamii

Mradi Wa EIC

ujenzi wa Kanisa Jipya

Kutokana na ongezeko la waumini na uhitaji wa nafasi ya kutosha kwa ajili ya ibada, uongozi wa Ebenezer International Church kupitia mkutano mkuu wa mwaka 2024 uliridhia kuanza rasmi mchakato wa ujenzi wa kanisa jipya. Lengo ni kuwa na jengo la kisasa litakalokidhi mahitaji ya huduma za kiroho na kijamii.

Ili kuhakikisha kuna nafasi ya kutosha kwa ujenzi wa jengo jipya na miundombinu ya ziada.

Ramani iliyosanifiwa kitaalamu ili kufanikisha ujenzi unaokidhi viwango vya kisasa.

Maandalizi ya makadirio ya gharama zote za ujenzi ili kurahisisha usimamizi wa rasilimali.

Hii ni pamoja na ruhusa za kisheria na kiutawala zinazohitajika kabla ya kuanza ujenzi.

Bishop Genoveva Charles Ntumo

Kiongozi Mkuu wa Kiroho wa Kanisa.

Mchungaji Joseph Godfrey Kihiyo

Naibu Askofu na Kiongozi wa Huduma.

Frank Chacha Nyantora

Kiongozi wa Idara ya Uongozi na Katibu wa Kanisa.

Frank Valence Mwabulambo

Kiongozi wa Idara ya Uinjilisti, Maombi na Maombezi.

Jeremiah Mutagoma

Kiongozi wa Idara ya Mipango na Ujenzi.

Sauli Hagayo

Mhasibu wa Kanisa na Kiongozi wa Idara ya Fedha

Tedy Filimon Jacobo

Kiongozi wa Idara ya Wanawake.

ALEX SHIJA

Kiongozi wa Idara ya Watoto na Vijana.